YOU ARE NOT ALONE

"I can’t give solutions to all of life’s problems, doubts, or fears. But I can listen to you, and together we will search for answers."

karibuni

Karibuni katika blog yetu ambayo itakuwa ikizungumzia kuhusu masuala ya uzazi hasa kwa wale wenye matatizo ya kuchelewa kupata watoto (infertility). Hapa tutajadili chanzo cha matatizo hayo na njia zinazoweza kutumika kuondoa tatizo hilo pamoja na kupeana ushauri na nasaha katika masuala mbalimbali yanayohusu uzazi. "KWA NEEMA YA MUNGU KILA MWANAMKE ATANYONYESHA"

Friday, 8 June 2012

MWEZI WA WASAKA DUNIANI

Katika post za mwanzoni niliwahi kueleza kuwa kuna  mwezi wa wasaka duniani, ambapo lengo kuu ni kutumia mwezi huu kusambaza elimu kwa jamii, kupeana faraja na kusaidiana kwa kila hali katika kupambana na tatizo la kukosa uzazi. baadhi ya nchi hutoa huduma za matibabu bure kwa wahitaji ama kupunguza kiwango cha malipo katika kutoa mchango wao kwa mwezi huu.
Katika kuzingatia umuhimu wa mwezi wetu huu nami nimeona  ni vizuri kuupa nafasi ya kipekee na kwa kuelimishana mambo mbali mbali yanayohusu kukosa uzazi (infertility). Hivyo basi napenda kutambulisha vipengele vipya ambavyo vitakuwa vinaelezea mambo mbali mbali yatakayotupa uelewa mzuri. Vipengele vipya ni kama ifuatavyo:- 

-FAHAMU KUKOSA UZAZI (INFERTILITY) - Tumekuwa tukiongea sana kuhusu suala hili la kukosa uzazi,  kusaka mtoto, kutafuta matibabu na mengineyo lakini je tunaelewa kwa undani maana yake, chanzo chake, na matibabu yake? kipengele hiki kitaelezea kwa undani kuhusu suala hilo.

-JINSI YA KUKABILIANA NA KUKOSA UZAZI (JKKU) - Hapa tutaeleza njia mbali mbali zinazoweza kumsaidia msaka kukabiliana na kupambana na hali halisi ili kuweza kumpunguzia machungu anayokutana nayo kwenye safari hii.

-NI CHAGUO LAKO, NI WAKO - Katika post zetu tunaongelea sana kuhusu kutafuta matibabu ili kuweza kupata mtoto wa kuzaa mwenyewe, lakini kuna wasaka wenzetu ambao wapo katika hali ambayo kupata mtoto wa kuzaa mwenyewe ni hali ngumu kidogo, ili kuwapa nafasi na kuwa pamoja nao kipengele hichi kitasaidia katika kufanya maamuzi pale mtu anapohitaji kuasili (adoption) mtoto. Na hivyo tunasema ni chaguo lako, ni wako.

-INFERTILITY NEWS - Hapa tutapata habari mbali mbali zinazohusu infertility zinazotokea sehemu yoyote duniani, lengo ni kupeana taarifa na kwenda na wakati kwa maendeleo yoyote yanayotokea duniani

-MYTH & MISCONCEPTION - Kumekuwa na mawazo tofauti yanayoelezwa kuhusu chanzo cha kukosa uzazi na matibabu yake ambayo yanajenga imani potofu katika jamii. kipengele hichi kitaelezea na kutoa ukweli wa mawazo hayo.

-ZIFAHAMU DAWA UTUMIAZO - Katika safari ya usaka tunatumia dawa za aina mbali mbali, lakini ukweli ni kwamba asilimia kubwa ya watanzania hatuna maelezo ya kutosha ya dawa tunazotumia na jinsi gani dawa hizo zinatusaidia, katika kipengele hiki utayapata yote hapo. Infertility Fighter kwa ajili yako.

ULIWAHI KUFAHAMU KAMA KUNA RIBBON INAYOHUSU INFERTILITY?? KAMA BADO  ICHEKI HAPO CHINI. KITU BLUE NA PINK (nadhani wanawakilisha boy na girl tunaowasaka). Nimeipenda na nitaitafutia nafasi kwa hapo juu niiweke

Monday, 28 May 2012

HAMASIKA

Fertility Success Stories

Zannyha's Story


Zannyha Martell
Home: Birmingham, Alabama
Child: 12 months


by Connie Matthissen
The first time Zannyha Martell became pregnant, it was a complete surprise. "We weren't even trying," she recalls. "I was 25, and I didn't feel ready to have a child. I thought, 'Wait, I'm too young to have a baby!'"
Zannyha, who moved to the United States from Mexico when she was a teenager, had what she calls a "perfect pregnancy" and an easy delivery — until the last minute, when her baby went into fetal distress and was born dead. "They couldn't find anything wrong," says Zannyha. "They think she may have choked on some phlegm."
After losing their baby, Zannyha and her husband, Miguel, decided to wait before trying again. Three years later, when they decided they were ready, Zannyha couldn't seem to get pregnant.
"It put such stress on our marriage. Sex was no longer fun — my husband was like a machine to me. It was like, 'come on, it's time, get over here!'"
The fertility specialists they consulted couldn't find anything wrong with either of them. One doctor suggested that Zannyha's weight might be impeding conception, so she dropped the extra pounds but still didn't get pregnant. Over the next five years, they sold their house and cashed in their retirement plans so they could afford fertility treatments. After two IVF procedures, she still wasn't pregnant.
"It was a terrible time," Zannyha says today. "It put such a stress on our marriage. Sex was no longer fun -- my husband was like a machine in my eyes. It was like, 'Come on, it's time, get over here!'"
Finally, the fertility specialist told the couple that, even though she could find no physical reason they could not bear a child, there was nothing more she could do. "I just don't think it's going to happen," she said.
"We were very sad," says Zannyha. "But by then, we'd pretty much given up hope."
Six or seven months after they stopped fertility treatments, Zannyha went to the doctor for a checkup. She was concerned because she was tired all the time and kept bursting into tears for no apparent reason. After running several tests, her doctor told her to sit down -- and informed her that she was eight weeks pregnant.
When Zannyha's husband, Miguel, walked in the door from work, she showed him the sonogram. Miguel had come up with the idea that Zannhya had a tumor -- that was what was preventing her from getting pregnant and making her tired -- so when he saw the sonogram, he assumed it was a picture of the tumor.
"When are they going to take it out?" he asked. When she told him it was a baby in the sonogram, not a tumor, he still didn't believe it.
Zannyha now thinks that her infertility was caused at least in part by the trauma of losing her first child. "I was so afraid of going through it all again, even though it was what I wanted more than anything," she says. "The first time, it was such an easy pregnancy, and everything went perfect. But if everything was perfect, how could my baby die? And could it happen all over again?"
Perhaps because she'd tried so hard and for so long, when she finally got pregnant, Zannyha was able to enjoy the experience completely. "I just felt joy and happiness the whole time," she says. "It was considered a high-risk pregnancy because I was 35 and what had happened before. But everything went fine." Gabriella was born in February 2007.
"I've loved every minute of being a mother," says Zannyha. "You hear people complaining about their kids, about getting up in the night, about flus and vomiting. But if you have trouble having a baby, you cherish every minute."

Friday, 25 May 2012

Safari ya Wasaka: GOOD NEWS

Wadau nina furaha kubwa sana kuwapa taarifa kuwa msaka mmoja kati yetu amepata POSITIVE PREGNANCY TEST RESULT. Habari hizi tayari zimeshathibishwa na daktari.
Kujua ni msaka yupi huyo na safari yake ilikuwaje, usicheze mbali na hapa nitakuletea profile yake, tusubiri kidogo baby wetu atulie tumboni si mwajua tena tulivyosaka!!!  Kwa niaba ya wasaka team, nachukua nafasi hii kukupongeza mpendwa wetu, mungu akusaidie na akukuzie mtoto wako, na akupe safari nyepesi hadi kujifungua salama bila ya matatizo. KWA NEEMA YA MUNGU KILA MWANAMKE ATANYONYESHA..... SAFARI BADO YAENDELEA....