YOU ARE NOT ALONE

"I can’t give solutions to all of life’s problems, doubts, or fears. But I can listen to you, and together we will search for answers."

karibuni

Karibuni katika blog yetu ambayo itakuwa ikizungumzia kuhusu masuala ya uzazi hasa kwa wale wenye matatizo ya kuchelewa kupata watoto (infertility). Hapa tutajadili chanzo cha matatizo hayo na njia zinazoweza kutumika kuondoa tatizo hilo pamoja na kupeana ushauri na nasaha katika masuala mbalimbali yanayohusu uzazi. "KWA NEEMA YA MUNGU KILA MWANAMKE ATANYONYESHA"

Saturday 25 February 2012

just a moment please

Wapendwa,
naomba mnivumilie kidogo tu muda si mrefu nitamalizia story yangu. nimepokea malalamiko mengi kuhusu kutomalizia story, naomba tuelewe kuwa lengo hapa ni kumsaidia mwanamke kwa kila njia, naweza kuandika story kwa mistari mitatu tu na nikamaliza, sawa itasaidia lakini sio wote kwani nitasema tu ilikuwaje nilifanya nini na ikawa nini. wakati kuna mwanamke mwenzetu ambaye yupo kwenye hali ngumu kumtoa hapo alipo na kumwambia aamini matokeo yako ni ngumu, pia lengo ni kusaidiana kupata kizazi na pia kimawazo na nasaha hata kwa wale ambao hawawezi kupata tena watoto.

pia tukumbuke kuwa blog yetu inagusa hisia nzito za watu, watu walioumia na wengine hata kukata tamaa ya maisha hivyo inabidi kujipanga kwa kila tutakaloongea ili mdau alipokee vizuri na liwe la msaada kwake ni kama mfano wa mtu mwenye ulemavu wa macho ukakurupuka na kumuita kipofu ni lazima ataumia ila ukitumia hilo la kwanza atakuelewa, hivyo uchaguzi wa maneno au lugha safi pia unachangia kuchelewa huko.

jambo lingine ni kuwa hapa naongelea historia ya maisha ya ukweli na sio hadithi ya kutunga wala maigizo ambayo inashirikisha watu wengi, inabidi kuwa makini pia na maelezo kwani pamoja na kuwa wapo na wanatukwaza kwa shida zetu hizi lakini bado pia watu hao ni sehemu ya maisha yetu na jamii inayotuzunguka hivyo pamoja na yote tunahitaji kuwa na mahusiano mema nao.

naomba tushirikiane kwa wale wote wenye maoni, michango au ushuhuda mniandikie kupitia e-mail yangu sanraznassy@hotmail.com nami nitayaweka hadharani ili kila mwanamke afaidike. muda si mrefu nitatoa namba ya simu tuwasiliane.

kwa wale wanaohitaji kujua siri yangu pliz nitumieni email pia mniandikie na contact zenu tutawasiliana. sio siri kubwa ila napenda kuongea nanyi private ili kulinda heshima za watu mbali mbali akiwemo mwenza wangu.

tushirikiane, pamoja tutashinda.

No comments:

Post a Comment