YOU ARE NOT ALONE

"I can’t give solutions to all of life’s problems, doubts, or fears. But I can listen to you, and together we will search for answers."

karibuni

Karibuni katika blog yetu ambayo itakuwa ikizungumzia kuhusu masuala ya uzazi hasa kwa wale wenye matatizo ya kuchelewa kupata watoto (infertility). Hapa tutajadili chanzo cha matatizo hayo na njia zinazoweza kutumika kuondoa tatizo hilo pamoja na kupeana ushauri na nasaha katika masuala mbalimbali yanayohusu uzazi. "KWA NEEMA YA MUNGU KILA MWANAMKE ATANYONYESHA"

Saturday 25 February 2012

Msapoti mwenza wako


tatizo la kushindwa kupata ujauzito linaweza kutokana na mwanamke au mwanaume, inaweza kuwa wote kwa pamoja au sababu nyenginezo. mara nyingi tatizo likiwa kwa mwanaume, mwanamke huwa na uvumilivu na upendo, humsubiria mwenziwe mpaka kieleweke!!! (ingawa wapo wachache wasioweza kuvumilia), lakini hali huwa tofauti iwapo tatizo ni la mwanamke. Ukweli ni kwamba ni wanaume wachache sana wanaoweza kuwavumilia na kuwasapoti wenza wao. wengi wao hushindwa kutokana na presha za familia zao au mazingira yanayowazunguka. wanachosahau ni kuwa kile kitendo cha kumnyanyapaa mwenzi wako kinaweza kuwa ndio sababu kubwa ya nyinyi kukosa mtoto kwani mwanamke huishia kuwa na msongo wa mawazo muda wote....



 kila mtu kivyake......



hupunguza upendo kwa kweli na humfanya mwanamke ajione kama ni mkosaji wakati hana hatia yoyote.
Daima kumbuka upendo wako ndio utakaomtia nguvu za kupambana na majaribu hayo.



cheki inavonoga mkiongozana wote kutafuta suluhisho

na kuyapokea majibu kwa pamoja jee!!!


jamani ni upendo wa hali ya juu. hata kama ni negative pliz kuwa karibu nae kwani anakuhitaji zaidi ya unavyofikiria. kuwa baba ni fahari kwako na jamii lakini kuwa mama pia ni life time experience ambayo kila mwanamke anaihitaji. sio kosa lake laiti ungejua ni kiasi gani anaumia kwa majibu hayo hayo yanayokukera wewe ungeisimamisha hata dunia isitembee mpaka machungu ya mwenzako yapungue.


usipomsaidia sasa hivi utajisikiaje siku mambo yakiwa mazuri?

siwezi kuimagine utakavyokuwa unajieleza..... oh darling nilijuwa tu tutafanikiwa. au mpenzi nimekuwekea pesa za shopping kwa ajili yako na baby wetu. duh hebu simama sasa na uchukue nafasi yako, mpende na umsapoti ili mambo yakijipa uwe proud kikweliiii hata ukijamuhadithia mwanao jinsi mlivyosubiri huwi na majuto


pliz show love...



daima kumbuka, anaumia kama wewe na anakuhitaji zaidi wewe ndio nguzo ya ujasiri na nguvu zake kwa pamoja mtayashinda majaribu, pliz do it for her na huyo baby unaemtamani....

napenda kuchukua nafasi hii kuwapa hongera wale wote wanaowafariji na kuwatia moyo wenza wao. huo ni ujasiri na kutimiza ahadi yako ya kumlinda, kumheshimu na kumpenda. naamini dini au imani zote wanazingatia hili wakati wanapofungisha ndoa, kwa waislamu huhimizwa kuwa na mapenzi (mawadda) kwa wake zao pamoja na huruma na wakristo pia huhimizwa mapenzi tena na viapo kupeana for better for worse. na imani zote nyinginezo naamini wanazingatia hili.


No comments:

Post a Comment